Mioyo yetu yaumia, ndoto zetu za
didimia,
Wakati wetu wa timia, duniani twapitia,
Swali langu kwa wakenya, mbona chuki kwa
wenzetu?
Usalama wa mwananchi, ni hekaya kwa Abunuasi
Ukijiburudisha kilabuni, kuamka kesho
jinamizi
Swali langu kwa wakenya, atakeyekufa
kesho nani?
Ukiamka asubuhi, kufika jioni shukrani
Ukitoka kazini, kufika nyumbani piga dua
Swali langu kwa Wakenya, wauaji hawa
kina nani?
Twapoteza wahitajika, kwa vinyweo
kadhalika
kwani kifo hakina huruma, kwa mkenya mheshimiwa
dua langu kwake Mola, laza roho zetu
pahali pema.
By:
Otieno Lawrence
©2016
No comments:
Post a Comment